Taarifa kutoka ofisi ya Waziri Mkuu ilisema kuwa utawala wa Kizayuni unakusudia kuhamishia mivutano na migogoro katika Bahari ya Mashariki ya Mediterania. Kupro, Ugiriki, na Israel badala ya kuimarisha amani, wanatafuta kuongeza migogoro ya kijeshi, jambo ambalo ni tishio kwa amani. Aliongeza kuwa unafiki wa Kupro ya Kusini kuunda ushirika wa kijeshi dhidi ya Uturuki utafanya utatuzi wa suala la Kupro kuwa mgumu.
Benjamin Netanyahu hivi karibuni alikutana na Waziri Mkuu wa Ugiriki na Rais wa Kupro huko Jerusalem kuimarisha ushirikiano wa usalama. Vyombo vya habari vya Kiebrania vinaripoti kuwa Tel Aviv, Ugiriki, na Kupro zinapanga kuunda kikosi cha kijeshi cha pamoja cha watu 2,500 katika visiwa vya Ugiriki na maeneo yanayokaliwa kwa mabavu ili kukabiliana na Uturuki.
Your Comment